Spika wa mabunge ya Afrika Mashariki wakutana jijini DSM

Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni mwenyekiti wa mkutano wa Jukwaa la Maspika wa Mabunge ya Afrika Mashariki, Mhe. Anne Makinda(katikati) azungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) juu ya uwepo wa mkutano huo hapa nchini. Wengine pichani toka kulia ni Mh. Justine Muturi(spika wa Bunge la Kenya), Mh.Rebecca Kadaga(Spika wa Bunge la Uganda), Mh.Donatille Mukabalisa(Spika wa Bunge la Rwanda) pamoja na Mh. Daniel Kidega(Spika wa Bunge la Afrika Mashariki).
Spika wa mabunge ya nchi za AFRIKA Mashariki wanakutana jijini DSM kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya nchi hizo likiwemo suala la kukabiliana na vitendo vya kigaidi vilivyoshuhudiwa kwa siku chache zilizopita.

Spika wa Bunge la TANZANIA ANNE MAKINDA amesema Mkutano huo ni jukwaa la kushughulikia masuala mbalimbali yanayolenga kuharakisha maendeleo miongoni mwa nchi wanachama.

Mkutano wa KUMI NA MOJA wa Maspika wa Mabunge ya Nchi za Afrika Mashariki hufanyika kila mwaka kwa utaratibu wa kubadilishana Uenyekiti ambapo safari hii Mwenyekiti ni Spika wa TANZANIA ANNE MAKINDA.

Post a Comment

0 Comments