WAKULIMA WA KAHAWA KUNUFAHIKA

Tokeo la picha la WAKULIMA WA KAHAWA
Kwa ufupi
Mkurugenzi Mtendaji Kampuni ya Chai Bora Kapila Ariyatilaka alisema hayo jana wakati wa uzinduzi wa bidhaa zitokanazo na kahawa.
Dar es Salaam. Wakulima wa kahawa nchini wataendelea kunufaika na zao hilo baada ya kuanzishwa kwa viwanda vya usindikaji.
Mkurugenzi Mtendaji Kampuni ya Chai Bora Kapila Ariyatilaka alisema hayo jana wakati wa uzinduzi wa bidhaa zitokanazo na kahawa.
Alisema wameingiza bidhaa mpya sokoni zitakazopanua wigo wa soko la kahawa na kuwanufaisha zaidi wakulima.
“Tumekuja kupanua wigo wa soko la kahawa, tuna mahitaji ya wastani wa tani 500 kwa mwezi, kwa ajili ya uzalishaji wa bidhaa zetu hususan ile ya Cafe Bora,” alisema na kuongeza:
“Lengo la kampuni ni kutosheleza mahitaji ya ndani pamoja na nchi za Afrika Mashariki.
Ariyatilaka alisema wakulima wa nyanya, pilipili na bidhaa nyingine pia wana fursa nzuri ya soko baada ya kampuni hiyo kuingia makubaliano ya kibiashara na Kampuni ya Dabaga iliyopo Iringa.
“Tunaangalia zaidi fursa ya masoko kwa bidhaa za mashambani kutokana na changamoto zinazowakabili wakulima, ndiyo maana tunashirikiana na Dabaga,” alisema.
Alisema iwapo bidhaa za Dabaga zitauzwa zaidi, mahitaji yataongezeka kwa wakulima wa nyanya Iringa na kwingineko.
“Tutakuwa tumewawezesha wakulima kuongeza kipato na pia Serikali itapata kodi zaidi kutokana na mauzo ,” alisema
Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa Kampuni ya Chai Bora, Martin Ng’ethe alisema Tanzania inajivunia kuwa na aina zote za kahawa.
Alizitaja kuwa ni Arabika na Robusta tofauti na nchi nyingine zenye aina mmoja ya kahawa.

Post a Comment

0 Comments